Swali: Kuhusu Takbiyr misikitini alete Takbiyr mtu mmoja na waitikie wengine baada yake?

Jibu: Kila mmoja alete Takbiyr kutegemea na hali yake. Hakuna Takbiyr za pamoja. Kila mmoja alete Takbiyr kivyake na haikusuniwa kuleta Takbiyr za pamoja. Kuleta Takbiyr kwa pamoja sio jambo limesuniwa. Hata hivyo kila mmoja alete Takbiyr kutegemea na hali yake. Sauti zikikutana haidhuru. Ama kupanga Takbiyr kuanzia mwanzo hadi mwisho wake kwa namna ya kwamba wakaanza na kumaliza kwa pamoja ni jambo halina msingi wowote.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/8774/حكم-التكبير-ايام-عيد-الاضحى-وصيغته
  • Imechapishwa: 15/06/2024