Swali: Nilisema “Allaahu Akbar” kwa ajili ya kutekeleza Sunnah kabla ya swalah ya Dhuhr na nikanuia kuiswali Rak´ah nne kwa Tasliym moja. Baada ya kumaliza kuswali Rak´ah moja kukakimiwa swalah. Je, nibadilishe nia na niswali Rak´ah mbili au niikate?
Jibu: Imethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ya kwamba amesema:
“Kunapokimiwa swalah basi hakuna swalah nyingine isipokuwa ile ya faradhi.”[1]
Ameipokea Muslim katika “as-Swahiyh” yake.
Kwa hiyo kilichowekwa katika Shari´ah pindi kunapokimiwa swalah na wewe waswali swalah iliyopendekezwa, basi uikate kutokana na Hadiyth hii tukufu.
Pia imesuniwa kwa muislamu kuswali swalah zilizopendekezwa Rak´ah mbilimbili; mchana na usiku. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Swalah ya usiku na mchana ni [Rak´ah] mbilimbili.”
Kuna maafikiano juu ya usahihi wake.
Imekuja katika upokezi ambao ni Swahiyh:
“Swalah ya usiku na mchana ni [Rak´ah] mbilimbili.”
Ameipokea Imaam Ahmad na watunzi wa as-Sunan kwa cheni ya wapokezi Swahiyh.
Lakini endapo swalah itakimiwa na yeye yuko katika Rukuu´ ya mwisho ya Sunnah au katika Sujuud ya mwisho bora ni kuikamilisha. Kwa sababu hakukubaki isipokuwa kitu kidogo kilicho chini ya Rak´ah. Uchache wa swalah ni Rak´ah moja.
[1] Ahmad (9563), Muslim (710) na Abu Daawuud (1266).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/389)
- Imechapishwa: 11/11/2021
Swali: Nilisema “Allaahu Akbar” kwa ajili ya kutekeleza Sunnah kabla ya swalah ya Dhuhr na nikanuia kuiswali Rak´ah nne kwa Tasliym moja. Baada ya kumaliza kuswali Rak´ah moja kukakimiwa swalah. Je, nibadilishe nia na niswali Rak´ah mbili au niikate?
Jibu: Imethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ya kwamba amesema:
“Kunapokimiwa swalah basi hakuna swalah nyingine isipokuwa ile ya faradhi.”[1]
Ameipokea Muslim katika “as-Swahiyh” yake.
Kwa hiyo kilichowekwa katika Shari´ah pindi kunapokimiwa swalah na wewe waswali swalah iliyopendekezwa, basi uikate kutokana na Hadiyth hii tukufu.
Pia imesuniwa kwa muislamu kuswali swalah zilizopendekezwa Rak´ah mbilimbili; mchana na usiku. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Swalah ya usiku na mchana ni [Rak´ah] mbilimbili.”
Kuna maafikiano juu ya usahihi wake.
Imekuja katika upokezi ambao ni Swahiyh:
“Swalah ya usiku na mchana ni [Rak´ah] mbilimbili.”
Ameipokea Imaam Ahmad na watunzi wa as-Sunan kwa cheni ya wapokezi Swahiyh.
Lakini endapo swalah itakimiwa na yeye yuko katika Rukuu´ ya mwisho ya Sunnah au katika Sujuud ya mwisho bora ni kuikamilisha. Kwa sababu hakukubaki isipokuwa kitu kidogo kilicho chini ya Rak´ah. Uchache wa swalah ni Rak´ah moja.
[1] Ahmad (9563), Muslim (710) na Abu Daawuud (1266).
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/389)
Imechapishwa: 11/11/2021
https://firqatunnajia.com/swalah-ya-sunnah-ni-rakah-mbilimbili-na-sio-nne/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)