Swali: Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Swalah ya mkusanyiko ni bora kwa daraja ishirini na saba kuliko anayeswali peke yake.”
Kuna wanaoitumia kama hoja kwamba swalah ya mkusanyiko imependekezwa tu. Je, utumiaji wao wa dalili ni sahihi?
Jibu: Hapana, si sahihi. Hadiyth inalenga tu fadhila za swalah ya mkusanyiko. Kuhusu hukumu yake inachukuliwa kutoka katika dalili zingine. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Mwenye kusikia adhaana na asiiendee hana swalah isipokuwa kama ana udhuru.” Kukasemwa: “Ni udhuru upi?” Akasema: “Woga au maradhi.”
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (41) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/ighastah%20%20-%204%20-%201%20-%201437.mp3
- Imechapishwa: 13/03/2017
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket