Ni lazima kuswali swalah ya ijumaa pasi na kujali imamu ni katika Ahl-us-Sunnah au Ahl-ul-Bid´ah au pasi na kujali ni mwema au mtenda dhambi. Haya yamesemwa na Ahmad. Imepokelewa kutoka kwa al-´Abbaas bin ´Abdil-´Adhwiym kwamba alimuuliza Abu ´Abdillaah [Ahmad bin Hanbal] kuhusu kuswali swalah ya ijumaa nyuma ya Mu´tazilah. Akasema:
“Mtu anatakiwa kushuhudia swalah ya ijumaa. Kama anajua kuwa swalah yake haisihi [kwa sababu ya ukafiri wao], basi atatakiwa kuirudi tena, na kama hajui kama ni sahihi au si sahihi, basi asiirudi upya.”
Ndipo nikamuuliza kwamba ikisemekana kuwa ameonelea kama walivoonelea. Akajibu:
“Mpaka awe na uhakika.”
Sijui kama kuna tofauti yoyote kwa wanachuoni juu ya hilo. Msingi wa hilo ni ueneaji wa maneno ya Allaah (Ta´ala):
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا نُودِيَ لِلصَّلَاةِ مِن يَوْمِ الْجُمُعَةِ فَاسْعَوْا إِلَىٰ ذِكْرِ اللَّـهِ
”Enyi walioamini! Inaponadiwa kwa ajili ya swalah siku ya ijumaa, basi kimbilieni katika utajo wa Allaah.”[1]
Vivyo hivyo maafikiano ya Maswahabah. ´Abdullaah bin ´Umar na Maswahabah wengine wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) walikuwa wakishuhudia swalah ya ijumaa pamoja na al-Hajjaaj na watu mfano wake. Haikupokelewa kutoka kwa mmoja katika wao kwamba alijitenga nao.
[1] 62:9
- Mhusika: Imaam Muwaffaq-ud-Diyn bin Qudaamah al-Maqdisiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Mughniy (3/169)
- Imechapishwa: 29/01/2021
Ni lazima kuswali swalah ya ijumaa pasi na kujali imamu ni katika Ahl-us-Sunnah au Ahl-ul-Bid´ah au pasi na kujali ni mwema au mtenda dhambi. Haya yamesemwa na Ahmad. Imepokelewa kutoka kwa al-´Abbaas bin ´Abdil-´Adhwiym kwamba alimuuliza Abu ´Abdillaah [Ahmad bin Hanbal] kuhusu kuswali swalah ya ijumaa nyuma ya Mu´tazilah. Akasema:
“Mtu anatakiwa kushuhudia swalah ya ijumaa. Kama anajua kuwa swalah yake haisihi [kwa sababu ya ukafiri wao], basi atatakiwa kuirudi tena, na kama hajui kama ni sahihi au si sahihi, basi asiirudi upya.”
Ndipo nikamuuliza kwamba ikisemekana kuwa ameonelea kama walivoonelea. Akajibu:
“Mpaka awe na uhakika.”
Sijui kama kuna tofauti yoyote kwa wanachuoni juu ya hilo. Msingi wa hilo ni ueneaji wa maneno ya Allaah (Ta´ala):
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا نُودِيَ لِلصَّلَاةِ مِن يَوْمِ الْجُمُعَةِ فَاسْعَوْا إِلَىٰ ذِكْرِ اللَّـهِ
”Enyi walioamini! Inaponadiwa kwa ajili ya swalah siku ya ijumaa, basi kimbilieni katika utajo wa Allaah.”[1]
Vivyo hivyo maafikiano ya Maswahabah. ´Abdullaah bin ´Umar na Maswahabah wengine wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) walikuwa wakishuhudia swalah ya ijumaa pamoja na al-Hajjaaj na watu mfano wake. Haikupokelewa kutoka kwa mmoja katika wao kwamba alijitenga nao.
[1] 62:9
Mhusika: Imaam Muwaffaq-ud-Diyn bin Qudaamah al-Maqdisiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Mughniy (3/169)
Imechapishwa: 29/01/2021
https://firqatunnajia.com/swalah-ya-ijumaa-nyuma-ya-ahl-ul-bidah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)