Swali: Mtu akiswali Dhuhr nyuma ya imamu anayeswali ´Aswr swalah yake ni sahihi?
Jibu: Mtu akiswali Dhuhr nyuma ya imamu anayeswali ´Aswr hakuna neno na swalah yake ni sahihi kwa mujibu wa maoni yenye nguvu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika kila kitendo kinategemea nia na kila mmoja atalipwa kwa lile alilonuia.”
Hakukuthibiti kitu kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kinachofahamisha ya kwamba nia ya imamu na mswaliji zinapaswa kuafikiana. Kwa hivyo kila mmoja anakuwa na nia yake kama inavyofahamisha Hadiyth:
“… na kila mmoja atalipwa kwa lile alilonuia.”
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/446)
- Imechapishwa: 23/07/2017
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)