Swali: Mtu akiswali Dhuhr nyuma ya imamu anayeswali ´Aswr swalah yake ni sahihi?
Jibu: Mtu akiswali Dhuhr nyuma ya imamu anayeswali ´Aswr hakuna neno na swalah yake ni sahihi kwa mujibu wa maoni yenye nguvu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika kila kitendo kinategemea nia na kila mmoja atalipwa kwa lile alilonuia.”
Hakukuthibiti kitu kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kinachofahamisha ya kwamba nia ya imamu na mswaliji zinapaswa kuafikiana. Kwa hivyo kila mmoja anakuwa na nia yake kama inavyofahamisha Hadiyth:
“… na kila mmoja atalipwa kwa lile alilonuia.”
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/446)
- Imechapishwa: 23/07/2017
Swali: Mtu akiswali Dhuhr nyuma ya imamu anayeswali ´Aswr swalah yake ni sahihi?
Jibu: Mtu akiswali Dhuhr nyuma ya imamu anayeswali ´Aswr hakuna neno na swalah yake ni sahihi kwa mujibu wa maoni yenye nguvu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika kila kitendo kinategemea nia na kila mmoja atalipwa kwa lile alilonuia.”
Hakukuthibiti kitu kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kinachofahamisha ya kwamba nia ya imamu na mswaliji zinapaswa kuafikiana. Kwa hivyo kila mmoja anakuwa na nia yake kama inavyofahamisha Hadiyth:
“… na kila mmoja atalipwa kwa lile alilonuia.”
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/446)
Imechapishwa: 23/07/2017
https://firqatunnajia.com/swalah-ya-anayeswali-dhuhr-nyuma-ya-anayeswali-aswr-ni-sahihi/