Swali: Sisi tunaishi katika moja ya nchi za kikafiri. Tuko wengi lakini misikiti ni michache. Tunapata ugumu katika kutekeleza swalah za ´iyd mbili. Hatuwezi kufanya swalah ya mkusanyiko mmoja kutokana na wingi wa watu. Vilevile hatuwezi kuswali nje ya msikiti. Je, tunaweza kutekeleza swalah ya ´iyd katika msikiti mmoja mara mbili au mara tatu kwa Khutbah yenye maudhui tofauti?
Jibu: Allaah (Jalla wa ´Alaa) amesema:
فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ
”Mcheni Allaah muwezavyo.”[1]
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Ninapokuamrisheni jambo basi lifanyeni muwezavyo.”[2]
Mkiweza kutekeleza swalah ya ´iyd kwa pamoja katika jangwani ndio Sunnah. Msipoweza basi inatosha wakipatikana miongoni mwenu watakaoweza kuhudhuria swalah hiyo.
[1] 64:16
[2] al-Bukhaariy (7288).
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ma´aalim Manhaj Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah, uk. 42
- Imechapishwa: 16/06/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
