Swali: Miji ambayo usiku au mchana unakuwa mrefu kwa mfano miezi sita. Vipi zitakuwa swalah na swawm zao?

Jibu: Miji ambayo usiku na mchana wake vinakuwa virefu, ikiwa wanapata usiku na mchana ndani ya masaa ishini na nne – hata kama moja kati ya hivyo kitakuwa kifupi – swalah za usiku wataziswali usiku hata kama sehemu ya usiku itakuwa fupi na swalah za mchana wataziswali mchana hata kama sehemu yake itakuwa ndefu. Hali kadhalika inapokuja katika swawm. Watafunga mchana na wafuturu usiku.

Ama ikiwa hawapati mchana na usiku ndani ya masaa ishirini na nne, watu hawa watafuata nchi iliokaribu zaidi na wao. Watachukua ratiba ya nchi ambayo iko karibu zaidi na wao ambayo iko na usiku na mchana. Haya ndio waliyofikia idara ya Fiqh na baraza la wanachuoni wakubwa.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (72) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1432-10-14.mp3
  • Imechapishwa: 21/08/2020