Siri za wanandoa haambiwi hata mzazi

 Swali: Je, imesihi kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Tafuteni msaada katika kutimiza haja zenu kwa kuzificha?”

Jibu: Hapana, hilo si Hadiyth ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Linapokewa kuwa ni katika maneno ya ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh).

Swali: Je, hili[1] linahusu siri kwa ujumla?

Jibu: Ni kuhusu siri ambazo kufichuliwa kwake kunaleta madhara na kunakhofiwa kwamba mwenye siri hataridhia kufichuliwa kwake, ni mamoja iwe ni kuhusu kujamiiana au jambo jingine.

Swali: Je, mwanamke anaruhusiwa kumwambia mama yake au dada yake?

Jibu: Hafai kufichua siri, si kwa mama yake wala kwa dada yake, hata kwa baba yake.

Swali: Ikiwa mwanamke huyu amepewa talaka na mwanaume, kisha mwanaume huyo anataka kumuoa mwanamke mwingine na mwanamke huyu anaogopa kwamba dada yake anaweza kudhurika?

Jibu: Siri haifichuliwi isipokuwa mwenye siri akiruhusu au sababu iliyokuwa inalazimisha kufichwa kwake iondoke.

[1] Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”Miongoni mwa watu waovu zaidi siku ya Qiyaamah ni mwanamume anayekaribiana na mke wake na mke anamkaribia, kisha anasambaza siri yake.” (Muslim)

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/audios/2555/232-من-باب-حفظ-السر
  • Imechapishwa: 11/03/2026