Swali: Ni jambo linalotambulika kwamba Shaykh Ibn Baaz (Rahimahu Allaah) amesema kuwa wanazuoni waliowapa udhuru waabudia makaburi kutokana na ujinga kwamba wamefahamu kimakosa masuala hayo na hivyo mtu anatakiwa kuwapambanulia mambo. Lakini wanazuoni hawa wakiendelea kuwapa udhuru watu hawa baada ya hoja kuwawia wazi…

Jibu: Tuletee maneno ya Shaykh Ibn Baaz. Tuletee maandiko tuyasome hapa. Baada ya hapo ndipo tutatazama maneno yako unayosema. Wanazuoni wana heshima yao. Usiwanasibishie kitu isipokuwa kwa marejeo yanayothibitisha yale mnayoyasema. Haijuzu kumnukuu Shaykh kupitia watu wengine au kusimulia kwamba Shaykh amesema haya na yale kupitia watu wengine. 

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ad-Durr an-Nadhwiyd (11) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/al_durr_15_03_1433.mp3
  • Imechapishwa: 29/05/2021