Swali 132: Je, ni kweli kwamba wanawake ndio wakazi wengi wa Motoni? Kwa nini iwe hivo?
Jibu: Ni kweli. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwaambia wakati alipokuwa anawatolea Khutbah:
“Enyi kongamano la wanawake! Toeni swadaqah. Kwani hakika mimi nyinyi ndio wakazi wengi wa Motoni.”
Kumepokelewa kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) utatizi huu ulioulizwa na muulizaji: “Tukasema: “Kwa nini, ee Mtume wa Allaah?” Akasema:
“Mnakithirisha laana na mnakufuru wema.”
Akasababisha (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) sababu ya kuwa kwao wengi Motoni. Kwa sababu wanakithirisha laana, matusi na maapizo na wanakufuru wema ambao ni yule mume. Ndio maana wakawa wakazi wengi wa Motoni.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa al-Mar´ah al-Muslimah, uk. 533
- Imechapishwa: 14/08/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)