Swali: Ni ipi Radd kwa mwenye kusema kwamba kuigawa Tawhiyd aina tatu ni kujifananisha na wakristo katika imani yao ya utatu?
Jibu: Ulinzi unatafutwa kwa Allaah. Anafananisha ´Aqiydah ya Tawhiyd na imani ya utatu? Haya yamo katika Qur-aan. Aina tatu za Tawhiyd zimechukuliwa kutoka katika Qur-aan. Aayah zote zinazozungumzia juu ya matendo ya Allaah na uwezo Wake ni Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah. Aayah zote zinazozungumzia juu ya kumuabudu Allaah ni Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah. Aayah zote zinazozungumzia juu ya majina na sifa za Allaah ni Tawhiyd-ul-Asmaa´ was-Swifaat. Aina tatu hizi zimetolewa katika Qur-aan. Lakini huyu ima ni mjinga au anajifanya kukosea na vilevile ni mpotevu ambaye analenga kukosea. Haya yanapatikana katika Qur-aan kwa kupitia tafiti za kisomi.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Furqaan (05) http://alfawzan.af.org.sa/node/2048
- Imechapishwa: 26/11/2016
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)