Jipime maarifa yako kuhusu twahara na swalah
Chemsha Bongo ya twahara na swalah 09
15:00
Kwanini Mtume alikuwa anachukizwa na watu kukaa na kuzungumza baada ya Ishaa?
- Kwa.s wasikose Fajr
- Kwa.s ni madhara kuzungumza wakati huo
- Kwa.s ni wakati wa wanandoa kufanya 'ibaadah
Ni ipi hukumu ya mswaliji kutazama juu wakati amesimama?
- Inafaa
- Haifai imekatazwa
- Ni Sunnah
Rawaatib ambazo Mtume amesema anayedumu kuziswali kila siku basi atajengewa nyumba Peponi ni ngapi?
- Ni 16 au 8
- Ni 20 au 15
- Ni 12 au 10
Ni vipi hukumu ya mwenye kupangusa shingo wakati wa kutawadha?
- Ni Sunnah
- Ni lazima kufanya hivo wakati wa kupangusa kichwa
- Ni Bid´ah
Atakayeamka wakati jua lachomoza ataanza Sunnah ya Fajr au faradhi kwanza?
- Faradhi kwanza
- Hatoswali tena muda umeshatoka
- Sunnah kwanza
Je, imesuniwa kwa ambaye ataswali Fajr baada ya jua kuchomoza kusoma kwa sauti ya juu?
- Hapana, kwa.s mchana umeshaingia
- Ndio, imesuniwa kufanya hivo
- Akisoma kwa sauti ya juu swalah haisihi
Ni ipi hukumu ya kwenda sambamba na imamu katika Takbiyr za swalah?
- Inafaa
- Haifai imekatazwa
- Ni Sunnah
Vipi wudhuu wa ambaye amegusa tupu ya mtoto wakati wa kumsafisha?
- Hana wudhuu'
- Sahihi ni kwamba wudhuu' wake upo
- Lazima atawadhe tena
Ni swalah ipi katika hizi ambayo inafaa kwa msafiri kuiswali kwa kutoelekea Qiblah?
- Swalah ya Tarawiyh peke yake
- Swalah ya Witr
- Swalah yoyote ya Sunnah
Je, inafaa kulipa swalah ya Sunnah iliyokupita?
- Ndio, km ulikuwa na ada kuiswali
- Hapana, haifai kabisa
- Inafaa tu ya kulipa zile Rawaatib
Je, inafaa kwa mwanamke kuswali swalah ya kupatwa kwa jua nyumbani kwake?
- Ndio, inafaa
- Hapana, nyumbani haifai ni msikitini tu
- Inafaa tu kama hawezi kwenda msikitini
Ni Sunnah zipi ambazo Mtume alikuwa haziachi safarini na katika hali ya ukazi?
- Istikhaarah, Dhuhaa na Raatibah ya Maghrib
- Witr tu
- Raatibah ya Fajr na Witr
Je, swalah ya Aswr ina Rakah ngapi za Sunnah kabla yake na malipo yake ni yepi?
- Rak'ah 2 na malipo yake ni Pepo
- Rak'ah 2 na malipo yake ni kujengewa mti Peponi
- Rak'ah 4 na Mtume amemuombea rehema
Ni ipi hukumu ya mwenye kusahau akaongea mazungumzo ya kidunia ndani ya swalah?
- Sahihi ni kwamba swalah yake haibatiliki
- Swalah inaharibika tu ikiwa ni ya faradhi
- Swalah yake ina mapungufu
Ni ipi hukumu ya kunyanyua mikono wakati wa kila Takbiyr?
- Ni Sunnah
- Ni lazima kufanya hivo
- Ni nguzo ya swalah isiyoachwa
Je, wakati wa dharurah mtu anaweza kuswali ndani ya kanisa?
- Hapana, mtu anakufuru
- Ndio, anaweza
- Anaweza tu kama ni swalah ya Sunnah na si faradhi
Je, mtu anatakiwa kutoa salamu wakati anapovunja swalah yake?
- Ndio, lazima atoe salamu
- Hakuna haja ya salamu, atatoka tu
- Atatoa salamu tu kama ameshafika Tashahhud
Ni wapi anaposimama mwanamke anayewaswalisha wanawake wenzake?
- Mbele yao
- Kokote tu muhimu aswali
- Katikati ya safu yao
Ni lini mtu anatakiwa kusujudu sijda ya kushukuru?
- Wakati anapopata neema
- Wakati wa kupata mtoto mchanga tu na vinginevyo
- Wakati wa kujadidikiwa na neema au kusalimishwa na balaa
Je, inafaa kwa maamuma anayeswali Aswr kumfuata imamu anayeswali Dhuhr au kinyume chake?
- Hapana haifai
- Ndio inafaa, kila mmoja kwa nia yake
- Swalah ya maamuma haisihi
Vipi wudhuu wa ambaye amegusa utupu wake?
- Ni sawa na haina neno
- Sahihi ni kwamba umechenguka kama ni kwa matamanio
- Anapata dhambi
Je, inafaa kwa msafiri kuanza kufupisha swalah kabla ya kutoka ndani ya mji wake?
- Ndio, inafaa
- Hapana, haifai
- Ndio Sunnah kufanya hivo