Jipime maarifa yako kuhusu twahara na swalah

Chemsha Bongo ya twahara na swalah 09

15:00

Kwanini Mtume alikuwa anachukizwa na watu kukaa na kuzungumza baada ya Ishaa?

Ni ipi hukumu ya mswaliji kutazama juu wakati amesimama?

Rawaatib ambazo Mtume amesema anayedumu kuziswali kila siku basi atajengewa nyumba Peponi ni ngapi?

Ni vipi hukumu ya mwenye kupangusa shingo wakati wa kutawadha?

Atakayeamka wakati jua lachomoza ataanza Sunnah ya Fajr au faradhi kwanza?

Je, imesuniwa kwa ambaye ataswali Fajr baada ya jua kuchomoza kusoma kwa sauti ya juu?

Ni ipi hukumu ya kwenda sambamba na imamu katika Takbiyr za swalah?

Vipi wudhuu wa ambaye amegusa tupu ya mtoto wakati wa kumsafisha?

Ni swalah ipi katika hizi ambayo inafaa kwa msafiri kuiswali kwa kutoelekea Qiblah?

Je, inafaa kulipa swalah ya Sunnah iliyokupita?

Je, inafaa kwa mwanamke kuswali swalah ya kupatwa kwa jua nyumbani kwake?

Ni Sunnah zipi ambazo Mtume alikuwa haziachi safarini na katika hali ya ukazi?

Je, swalah ya Aswr ina Rakah ngapi za Sunnah kabla yake na malipo yake ni yepi?

Ni ipi hukumu ya mwenye kusahau akaongea mazungumzo ya kidunia ndani ya swalah?

Ni ipi hukumu ya kunyanyua mikono wakati wa kila Takbiyr?

Je, wakati wa dharurah mtu anaweza kuswali ndani ya kanisa?

Je, mtu anatakiwa kutoa salamu wakati anapovunja swalah yake?

Ni wapi anaposimama mwanamke anayewaswalisha wanawake wenzake?

Ni lini mtu anatakiwa kusujudu sijda ya kushukuru?

Je, inafaa kwa maamuma anayeswali Aswr kumfuata imamu anayeswali Dhuhr au kinyume chake?

Vipi wudhuu wa ambaye amegusa utupu wake?

Je, inafaa kwa msafiri kuanza kufupisha swalah kabla ya kutoka ndani ya mji wake?