Jipime maarifa yako kuhusu swawm
Chemsha Bongo ya Ramadhaan 05
15:00
Ni ipi hukumu ya muislamu asiyefunga Ramadhaan bila udhuru wowote?
- Ni kafiri
- Ni mtenda dhambi kubwa
- Ni mtenda dhambi ndogo
Ni ipi kafara ya mfungaji aliyefanya tendo la ndoa na mkewe mchana wa Ramadhaan?
- Kulisha chakula masikini 10
- Kuacha huru mtumwa
- Kufunga siku 40 kwa mfululizo
Ni ipi hukumu ya swawm ya ambaye kumeadhiniwa Fajr akiwa na chakula mdomoni?
- Amefungua na lazima afunge siku nyingine badala yake
- Aendelee kula ila afanye haraka kumaliza
- Ameze kilichomo tayari mdomoni mwake ila asichukue kingine na swawm yake ni sahihi
Je, mtu anaweza kukaa Itikaaf miezi mingine nje ya Ramadhaan?
- Ndio, anaweza
- I'tikaaf inakuwa mwezi wowote kwa aliyefunga tu
- Hapana, hawezi
Je, inafaa kutegemea Hesabu juu ya kuanza na kumalizika mwezi wa Ramadhaan?
- Inafaa haina neno
- Inachukiza kufanya hivo kila mwaka
- Haifai, waislamu wanategemea kuangalia mwezi
Ni lini kuna matarajio makubwa zaidi ya kupata usiku wa Qadr?
- Tarehe 10 Ramadhaan
- Zile nyusiku za witiri khaswa usiku wa 27 Ramadhaan
- Tarehe 30 Ramadhaan
Ambaye hakufunga Ramadhaan anaweza kukaa Itikaaf?
- Hapana kabisa
- Anaweza na hakuna mahusiano kati ya hayo mawili
- Anaweza tu kama amefunga
Ni lini unaanza muda wa Itikaaf?
- Fajr ya tarehe 1 Ramadhaan
- Fajr ya tarehe 27 Ramadhaan
- Baada ya swalah ya Fajr tarehe 21 Ramadhaan
Ni ipi hukumu ya mnyonyeshaji asiyeweza kufunga Ramadhaan?
- Ataacha huru mtumwa juu ya kila siku aliyokula
- Ni lazima afunge kwa hali yoyote
- Baba wa mtoto atamsaidia kufunga
- Kama anachelea nafsi yake na mtoto wake atalipa na kulisha masikini mmoja kwa kila siku aliyofungua
Ni ipi hukumu ya mjamzito asiyeweza kufunga Ramadhaan?
- Kama anachelea nafsi yake na mtoto wake atalipa na kulisha masikini mmoja kwa kila siku aliyofungua
- Atafunga badala yake siku 60
- Atalisha masikini wawili kwa kila siku moja aliyokula
- Ni lazima afunge kwa hali yoyote
Imesuniwa kusema nini baada ya swalah ya Witr?
- Alhamdulillaah wa swalaatu was-Salaam 'alaa Rasuulillaah
- Astaghfirullaah mara 3
- Subhaana Malikul qudduus mara 3, kisha Rabbul Malaaikati war-Ruuh mara 1
Inafaa kuswali Rakah tatu za Witr kwa salamu moja?
- Hapana, haifai
- Inafaa tu kama amechoka sana
- Ndio, inafaa
Ni ipi hukumu ya swawm ya aliyetapika?
- Andelee na swawm yake kwani hakukusudia
- Afungue na badala yake afunge siku nyingine
- Huyo ni mgonjwa na lazima afungue
Inafaa kwa mwenye udhuru wa kufunga (kama mwenye hedhi) kula hadharani mchana wa Ramadhaan?
- Hapana haifai, ale kwa kujificha
- Inafaa kwani yuko na udhuru wa kishari'ah
- Inafaa tu kula jua likishazama
Ni wapi mtu anatakiwa kukaa Itikaaf?
- Nyumbani
- Msikitini
- Kote tu ni sawa
Je, inafaa kufunga siku ya shaka kwa ajili ya kuchukua tahadhari?
- Haijuzu ila kwa aliyezowea kufunga hapo kabla
- Inajuzu na hakuna ubaya wowote
- Swawm ni ´ibaadah kubwa na hivyo inapendeza
Ni yepi malipo ya mwenye kusimama usiku wa Qadr kwa imani na matarajio?
- Ni sawa na aliyehiji na Mtume
- Ataingia Peponi bila ya hesabu
- Atasamehewa madhambi yake yaliyotangulia
Inafaa kujifunika shuka moja na mke mchana wa Ramadhaan?
- Haifai kabisa
- Inafaa haina neno
- Inafaa tu kama wanandoa wote hawakufunga
Je, inafaa kwa mwenye kukaa Itikaaf kutoka msikitini?
- Ndio, inafaa kwa hali yoyote
- Hapana, ila kama kuna dharurah
- Ndio, ila asifanye masaa mengi nje ya msikiti
Nini imesuniwa kusema kwa mwenye kukutukana ilihali umefunga?
- Nawe mtukane kama yeye ndiye kakuanza
- Mwambie "Salaam!"
- Mwambie "Mimi nimefunga!"
Ni lini unaisha muda wa Itikaaf?
- Aswr ya tarehe 15 Ramadhaan
- Dhuhr ya tarehe 27 Ramadhaan
- Kuzama kwa jua ile siku ya mwisho ya Ramadhaan
Ni upi usahihi wa Hadiyth inayosema kumi la kwanza la Ramadhaan ni la rehema, la pili ni la msahama na la tatu kuachwa huru na Moto?
- Swahiyh
- Dhaifu
- Ni maneno ya Swahabah
- Ni maneno ya wanazuoni