Swali: Ni jambo limeenea siku hizi picha za sanamu juu ya baadhi ya majengo. Miongoni mwazo ni picha ya simba katika nembo ya saa za Orient, kaskazini mwa msikiti huu na mengineyo. Je, ni ipi hukumu ya hilo?
Jibu: Haijuzu kuchukua picha, si za wanyama wa mifugo wala za wanaadamu, si juu ya nyumba wala juu ya visivyo nyumba, kama milango na yanayofanana na milango. Bali ni wajibu kukataza jambo hili. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Usiache picha yoyote isipokuwa uifute.”
Amekataza (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) picha katika nyumba au kuzitengeneza. Kwa hiyo haijuzu kuning’iniza picha juu ya kuta, si sanamu wala zisizo sanamu. Ni wajibu kukataza jambo hili. Vilevile ni lazima kuwafikishia watawala jambo hili la maovu. Ni lazima kuwafikishia watawala na tujitegemee katika kuondoa jambo hili.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1483/حكم-الصور-المجسمة-من-الحيوانات
- Imechapishwa: 21/12/2025
Swali: Ni jambo limeenea siku hizi picha za sanamu juu ya baadhi ya majengo. Miongoni mwazo ni picha ya simba katika nembo ya saa za Orient, kaskazini mwa msikiti huu na mengineyo. Je, ni ipi hukumu ya hilo?
Jibu: Haijuzu kuchukua picha, si za wanyama wa mifugo wala za wanaadamu, si juu ya nyumba wala juu ya visivyo nyumba, kama milango na yanayofanana na milango. Bali ni wajibu kukataza jambo hili. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Usiache picha yoyote isipokuwa uifute.”
Amekataza (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) picha katika nyumba au kuzitengeneza. Kwa hiyo haijuzu kuning’iniza picha juu ya kuta, si sanamu wala zisizo sanamu. Ni wajibu kukataza jambo hili. Vilevile ni lazima kuwafikishia watawala jambo hili la maovu. Ni lazima kuwafikishia watawala na tujitegemee katika kuondoa jambo hili.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1483/حكم-الصور-المجسمة-من-الحيوانات
Imechapishwa: 21/12/2025
https://firqatunnajia.com/picha-za-masanamu-ya-wanyama/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket