Swali: Je, picha inaweza kusimamisha hoja dhidi ya mzinifu?

Jibu: Hapana, haijuzu kupiga picha. Picha ni haramu na haithibitishi upelelezi juu ya mtu. Lakini wakipatikana mashahidi wanne waliomuona, hapahitajiki picha. Kwa sababu kupiga picha ni shari kubwa.

Swali: Vipi ikiwa mtu ataleta picha na watu wakaiona?

Ibn Baaz: Hili ni jambo linalohitaji kuangaliwa vyema. Allaah (Jalla wa ´Alaa) amesema:

وَالَّذِينَ يَرْمُونَ الْمُحْصَنَاتِ ثُمَّ لَمْ يَأْتُوا بِأَرْبَعَةِ شُهَدَاءَ فَاجْلِدُوهُمْ ثَمَانِينَ جَلْدَةً وَلَا تَقْبَلُوا لَهُمْ شَهَادَةً أَبَدًا ۚ وَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْفَاسِقُونَ

“Wale wanaowasingizia [machafu] wanawake watwaharifu kisha hawaleti mashahidi wanne, basi wapigeni mijeledi themanini na wala msipokee ushahidi wao abadani – na hao ndio mafasiki.”[1]

Hili ni jambo linalohitaji kuangaliwa vyema. Wengi wengi wanaweza kutengeneza picha… mpiga picha anaweza kudanganya bila ya kumuona mpigwaji na hivyo akatengeneza picha yake. Qur-aan imetaja kuleta mashahidi wanne.

[1] 24:04

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/30951/هل-يجوز-اقامة-حد-الزنا-بدلالة-التصوير
  • Imechapishwa: 17/09/2025