Nijengee kaburi la baba yangu ikiwa mji wetu hawawaheshimu wafu?

Swali: Je, inafaa nijenge juu ya kaburi la baba yangu ikiwa ninaogopa kudhalilishwa kwa sababu mahali anapozikwa hawawaheshimu wafu na kuwashauri hakufai?

Jibu: Haijuzu kwa mtu yeyote kujenga juu ya kaburi la baba yake wala kaburi la yeyote mwingine. Inatakiwa azikwe pamoja na waislamu wengine katika makaburi ya waislamu na hilo linatosha. Haifai kwake kujenga juu ya kaburi la baba yake, kaburi la babu yake wala mtu mwingine yeyote. Ndivyo walivyofanya Maswahabah na waliokuja baada yao. Walizika maiti wao katika makaburi na hawakujenga juu ya makaburi. Hilo ndilo la wajibu.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1139/هل-يجوز-البناء-على-القبر-ان-خاف-عليه-من-الاهانة
  • Imechapishwa: 31/01/2026