Swali: Ni mapendekezo yepi ya I´tikaaf?
Jibu: Imependekezwa kwa mtu kujishughulisha na kumtii Allaah (´Azza wa Jall) katika kusoma Qur-aan, kuleta Adhkaar, kuswali na mengineyo. Asipoteze muda wake katika yasiyokuwa na faida kama wanavyofanya baadhi ya wafanyao I´tikaaf. Utawaona wanabaki msikitini na kila wakati wanajiwa na watu wanaomzungumzisha na wanakata I´tikaaf zao bila ya faida yoyote. Ama kuzungumza wakati fulani pamoja na baadhi ya watu na baadhi ya familia hakuna neno. Hayo ni kutokana na yale yaliyothibiti katika “as-Swahiyh” ya al-Bukhaariy na ya Muslim ambapo Hafswah (Radhiya Allaahu ´anhaa) alimwendea Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na akazungumza nae kiasi cha saa moja kisha akaondoka zake kwenda nyumbani kwake.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (20/175)
- Imechapishwa: 21/06/2017
Swali: Ni mapendekezo yepi ya I´tikaaf?
Jibu: Imependekezwa kwa mtu kujishughulisha na kumtii Allaah (´Azza wa Jall) katika kusoma Qur-aan, kuleta Adhkaar, kuswali na mengineyo. Asipoteze muda wake katika yasiyokuwa na faida kama wanavyofanya baadhi ya wafanyao I´tikaaf. Utawaona wanabaki msikitini na kila wakati wanajiwa na watu wanaomzungumzisha na wanakata I´tikaaf zao bila ya faida yoyote. Ama kuzungumza wakati fulani pamoja na baadhi ya watu na baadhi ya familia hakuna neno. Hayo ni kutokana na yale yaliyothibiti katika “as-Swahiyh” ya al-Bukhaariy na ya Muslim ambapo Hafswah (Radhiya Allaahu ´anhaa) alimwendea Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na akazungumza nae kiasi cha saa moja kisha akaondoka zake kwenda nyumbani kwake.
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (20/175)
Imechapishwa: 21/06/2017
https://firqatunnajia.com/ni-yepi-yaliyopendekezwa-katika-itikaaf/