Swali: Ni mapendekezo yepi ya I´tikaaf?
Jibu: Imependekezwa kwa mtu kujishughulisha na kumtii Allaah (´Azza wa Jall) katika kusoma Qur-aan, kuleta Adhkaar, kuswali na mengineyo. Asipoteze muda wake katika yasiyokuwa na faida kama wanavyofanya baadhi ya wafanyao I´tikaaf. Utawaona wanabaki msikitini na kila wakati wanajiwa na watu wanaomzungumzisha na wanakata I´tikaaf zao bila ya faida yoyote. Ama kuzungumza wakati fulani pamoja na baadhi ya watu na baadhi ya familia hakuna neno. Hayo ni kutokana na yale yaliyothibiti katika “as-Swahiyh” ya al-Bukhaariy na ya Muslim ambapo Hafswah (Radhiya Allaahu ´anhaa) alimwendea Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na akazungumza nae kiasi cha saa moja kisha akaondoka zake kwenda nyumbani kwake.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (20/175)
- Imechapishwa: 21/06/2017
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket