Swali: Kuna msafiri ambaye ilikuwa awaswalishe wakazi, akawaswalisha Dhuhr Rak´ah nne. Allaah (Ta´ala) amesema:
وَإِذَا ضَرَبْتُمْ فِي الْأَرْضِ فَلَيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ أَن تَقْصُرُوا مِنَ الصَّلَاةِ
“Mtakaposafiri katika ardhi basi si dhambi kwenu kufupisha swalah.”[1]
Kitendo chake ameenda kinyume na Sunnah?
Jibu: Ndio, ameenda kinyume na Sunnah, kwa sababu haikuthibiti kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikamilisha swalah safarini. ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesema:
“Makkah swalah ilifaradhishwa Rak´ah mbili. Baada ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuhajiri al-Madiynah zikaongezwa Rak´ah zingine mbili isipokuwa Maghrib ambayo ni witiri ya leo na Fajr kwa sababu ya kisomo chake kirefu. Wakati (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliposafiri akaswali ile swalah ya mwanzo.”[2]
Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) amesema:
“Swalah ya safari ni Rak´ah mbili. Zimeteremshwa kutoka mbinguni na yule mwenye kukataa anakufuru.”
Hili ni wajibu. Maoni sahihi ni kwamba ni wajibu kufupisha swalah. Sio ruhus peke yake, kama wanavosema Shaafi´iyyah. Wao wanaona kuwa kufupisha ni ruhusa na bora ni kuswali kikamilifu. Mambo sivyo hivyo. Ni lazima kufupisha kwa sababu haikuthibiti ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliswali kikamilifu alipokuwa safarini.
[1] 04:101
[2] al-Bukhaariy na Muslim.
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 297-298
- Imechapishwa: 27/04/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket