Swali: Ni sahihi ya kwamba hakuna kukatazana katika mambo yalio na tofauti?
Jibu: Kwanza ikiwa ni katika ´Aqiydah itambulike kuwa hakuna tofauti katika ´Aqiydah. Lililo la wajibu kwetu ni kufuata mdhehebu ya Salaf na tusiwe na tofauti. Mambo ya tofauti ikiwa yanahusiana na mambo ya Fiqh, yamegawanyika sehemu mbili:
1- Mambo ambayo dalili zimedhihirika katika moja ya kauli mbili. Ni wajibu kumzindua mwenye kwenda kinyume kwa kuwa dalili iko na yule mwingine. Inatakiwa kumuwekea wazi hili.
2- Ikiwa dalili haikudhihirika na kauli zote mbili zina nguvu, kuna uwezekano ikawa hivi na kuna uwezekano ikawa vile, wote wawili wawili hawakudhihirikiwa na dalili, hakuna kukemeana katika mambo ya Ijtihaad.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Aqiydat-is-Saffaariniyyah (07) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/sfranih_07.mp3
- Imechapishwa: 27/06/2018
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)