Swali: Mmoja wa ndugu amesema kuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) anadhulumiwa na akatumia dalili kwa maneno Yake (Ta´ala):
إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ
“Hakika shirki ni dhulma kubwa mno!”[1]
Kwa hivyo unapovuka mipaka ya Allaah basi, unakuwa umemdhulumu. Lakini dhuluma inayoendana Naye (Subhaanah). Je, maneno haya ni sahihi?
Jibu: Haifai kusema hivyo. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:
وَمَا ظَلَمُونَا وَلَـٰكِن كَانُوا أَنفُسَهُمْ يَظْلِمُونَ
”Hawakutudhulumu Sisi, lakini walikuwa wakizidhulumu nafsi zao.”[2]
Dhuluma ni kuweka kitu mahali pasipo pake. Haimdhuru Allaah chochote. Bali wao ndio wanaojidhulumu na kubeba athari ya matendo yao. Kwa sababu hii amesema:
وَمَا ظَلَمُونَا وَلَـٰكِن كَانُوا أَنفُسَهُمْ يَظْلِمُونَ
”Hawakutudhulumu Sisi, lakini walikuwa wakizidhulumu nafsi zao.”[3]
Dhuluma ni kuweka jambo mahali pasipo pake. Maasi ni dhuluma kwa nafsi na utiifu ni faraja kwake. Dhuluma zao na maasi yao havimdhuru Allaah, bali madhara yavyo ni dhidi yao:
إِنْ أَحْسَنتُمْ أَحْسَنتُمْ لِأَنفُسِكُمْ ۖ وَإِنْ أَسَأْتُمْ فَلَهَا
”Mkifanya wema basi mnanjifanyia wema kwa ajili ya nafsi zenu wenyewe, na mkifanya maovu basi ni dhidi yake.”[4]
مَّنْ عَمِلَ صَالِحًا فَلِنَفْسِهِ ۖ وَمَنْ أَسَاءَ فَعَلَيْهَا
”Yeyote atakayetenda mema, basi ni kwa ajili ya nafsi yake, na yeyote atakayefanya maovu, basi ni dhidi yake.”[5]
[1] 31:13
[2] 02:57
[3] 02:57
[4] 17:07
[5] 41:46
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/30983/ما-معنى-قوله-تعالى-ان-الشرك-لظلم-عظيم
- Imechapishwa: 19/09/2025
Swali: Mmoja wa ndugu amesema kuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) anadhulumiwa na akatumia dalili kwa maneno Yake (Ta´ala):
إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ
“Hakika shirki ni dhulma kubwa mno!”[1]
Kwa hivyo unapovuka mipaka ya Allaah basi, unakuwa umemdhulumu. Lakini dhuluma inayoendana Naye (Subhaanah). Je, maneno haya ni sahihi?
Jibu: Haifai kusema hivyo. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:
وَمَا ظَلَمُونَا وَلَـٰكِن كَانُوا أَنفُسَهُمْ يَظْلِمُونَ
”Hawakutudhulumu Sisi, lakini walikuwa wakizidhulumu nafsi zao.”[2]
Dhuluma ni kuweka kitu mahali pasipo pake. Haimdhuru Allaah chochote. Bali wao ndio wanaojidhulumu na kubeba athari ya matendo yao. Kwa sababu hii amesema:
وَمَا ظَلَمُونَا وَلَـٰكِن كَانُوا أَنفُسَهُمْ يَظْلِمُونَ
”Hawakutudhulumu Sisi, lakini walikuwa wakizidhulumu nafsi zao.”[3]
Dhuluma ni kuweka jambo mahali pasipo pake. Maasi ni dhuluma kwa nafsi na utiifu ni faraja kwake. Dhuluma zao na maasi yao havimdhuru Allaah, bali madhara yavyo ni dhidi yao:
إِنْ أَحْسَنتُمْ أَحْسَنتُمْ لِأَنفُسِكُمْ ۖ وَإِنْ أَسَأْتُمْ فَلَهَا
”Mkifanya wema basi mnanjifanyia wema kwa ajili ya nafsi zenu wenyewe, na mkifanya maovu basi ni dhidi yake.”[4]
مَّنْ عَمِلَ صَالِحًا فَلِنَفْسِهِ ۖ وَمَنْ أَسَاءَ فَعَلَيْهَا
”Yeyote atakayetenda mema, basi ni kwa ajili ya nafsi yake, na yeyote atakayefanya maovu, basi ni dhidi yake.”[5]
[1] 31:13
[2] 02:57
[3] 02:57
[4] 17:07
[5] 41:46
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/30983/ما-معنى-قوله-تعالى-ان-الشرك-لظلم-عظيم
Imechapishwa: 19/09/2025
https://firqatunnajia.com/ni-sahihi-kusema-kuwa-allaah-amedhulumiwa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
