Ni lini mswaliji anasimama na kukamilisha swalah yake?

Swali: Ni lini ninatakiwa kusimama na kukamilisha swalah wakati ninapopitwa na Rak´ah moja? Je, inakuwa wakati imamu anapomaliza kutoa Tasliym ya kwanza au baada ya kutoa zote mbili?

Jibu: Hapana, inakuwa baada ya kumaliza kutoa ya pili. Usisimame isipokuwa baada ya [imamu] kumaliza kutoa Tasliym ya pili kwa kuwa bado yumo ndani ya swalah.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (43) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1431-3-29.mp3
  • Imechapishwa: 21/08/2020