Swali: Ni ipi hukumu ya kuzipaka rangi nyeusi nywele?
Jibu: Haijuzu. Haijuzu kuzibadilisha nywele kwa rangi nyeusi. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Zibadilisheni mvi hizi na jiepusheni na rangi nyeusi.”
Abu Daawuud amepokea ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Katika mwisho wa zama watakuja watu ambao wanapaka rangi nyeusi kama kifua cha njiwa; hawatohisi harufu ya Pepo.”[1]
Haya ni matishio makali. Haijuzu kupaka nywele rangi nyeusi. Mvi zinabadilsihwa kwa rangi nyingine isiyokuwa nyeusi ikiwemo vilevile hina, katam na zafarani.
[1] al-Albaaniy amesema:
”Ameipokea Abu Daawuud, an-Nasaa’iy, Ahmad, adh-Dhwiyaa’ al-Maqdisiy katika ”al-Mukhtaarah” na wengine wengi ambao hakuna nafasi ya kuwataja. Mlolongo wa wapokezi wake ni Swahiyh na iko kwa masharti ya al-Bukhaariy na Muslim.” (Ghaayat-ul-Maraam, uk. 70-71)
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (82) http://alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/Ighastah-08-3-1439-01.mp3
- Imechapishwa: 11/02/2018
Swali: Ni ipi hukumu ya kuzipaka rangi nyeusi nywele?
Jibu: Haijuzu. Haijuzu kuzibadilisha nywele kwa rangi nyeusi. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Zibadilisheni mvi hizi na jiepusheni na rangi nyeusi.”
Abu Daawuud amepokea ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Katika mwisho wa zama watakuja watu ambao wanapaka rangi nyeusi kama kifua cha njiwa; hawatohisi harufu ya Pepo.”[1]
Haya ni matishio makali. Haijuzu kupaka nywele rangi nyeusi. Mvi zinabadilsihwa kwa rangi nyingine isiyokuwa nyeusi ikiwemo vilevile hina, katam na zafarani.
[1] al-Albaaniy amesema:
”Ameipokea Abu Daawuud, an-Nasaa’iy, Ahmad, adh-Dhwiyaa’ al-Maqdisiy katika ”al-Mukhtaarah” na wengine wengi ambao hakuna nafasi ya kuwataja. Mlolongo wa wapokezi wake ni Swahiyh na iko kwa masharti ya al-Bukhaariy na Muslim.” (Ghaayat-ul-Maraam, uk. 70-71)
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (82) http://alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/Ighastah-08-3-1439-01.mp3
Imechapishwa: 11/02/2018
https://firqatunnajia.com/ni-ipi-hukumu-ya-kuzipaka-nywele-rangi-nyeusi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)