Ni ipi hukumu ya adhaana kwa wasafiri?

Swali: Ni ipi hukumu ya adhaana kwa wasafiri?

Jibu: Wanazuoni wametofautiana juu ya jambo hili. Maoni ya sawa ni kwamba ni wajibu kwa safiri kuadhini. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwambia Maalik bin al-Huwayrith (Radhiya Allaahu ´anh) pindi walipokuwa wanasafiri kutokea nyumbani kwake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

“Utapofika wakati wa swalah, basi aadhini mmoja wenu na mkubwa wenu aswalishe.”[1]

Jengine ni kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kamwe hakuach kuadhini wala kukimu, ni mamoja katika hali ya safari wala ya wenyeji. Alikuwa akimwamrisha Bilaal (Radhiya Allaahu ´anh) aadhini wakati wa safari yake.

[1] al-Bukhaariy (628).

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/160)
  • Imechapishwa: 22/05/2026