Kuadhini kabla ya kuingia wakati

Swali: Je, adhaana kabla ya wakati inasihi?

Jibu: Adhaana kabla ya wakati haisihi. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Utapofika wakati wa swalah, basi aadhini mmoja wenu na mkubwa wenu aswalishe.”[1]

Swalah haiwezi kuswaliwa isipokuwa baada ya kuingia wakati. Hadiyth ni yenye kuenea na haikubagua kitu. Haipingani na Hadiyth inayosema:

“Bilaal anaadhini usiku ili arudi anayeswali katika nyinyi na aamke anayelala katika nyinyi.”[2]

Inafahamisha kuwa adhaana ya Bilaal sio kwa ajili ya swalah Fajr.

[1] al-Bukhaariy (628).

[2] al-Bukhaariy na Muslim.

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/189)
  • Imechapishwa: 22/05/2026