Namna hii ndio al-Halabiy anavyomtetea al-Maghraawiy na al-Ma´ribiy

al-Halabiy amesema:

“Mambo hayatakiwi kuwa namna hii kwa njia ya kwamba mtu akawapatia mtihani wengine kwa kuwatumia watu na kusababisha tofauti kwa sababu ya wengine. Mtihani kama huo unatakiwa kuwa tu kwa mtu ambaye Ahl-us-Sunnah na wanachuoni wao wamekubaliana juu ya kujeruhiwa na kukemewa au kusifiwa na kutapwa. Sidhani kama hali ni hivyo kwa watu hawa wawili – al-Maghraawiy na al-Ma´ribiy – na wale wenye kufuata nyayo zao.”

Si Abul-Hasan wala al-Maghraawiy so katika Ahl-us-Sunnah. Wanachuoni wa Ahl-us-Sunnah hawakukubaliana kabisa juu ya kwamba wasikaripiwe kwa sababu wameshikamana na Sunnah, kuifuata Sunnah na kuita kwayo. Vitabu vyao na matendo yao yanatolea dalili kuonyesha jinsi walivyo mbali kabisa na Sunnah. Sijui ni vipi unaweza kujifikiria kitu kama hicho.

Huoni jinsi Abul-Hasan anavyokataa maelezo yaliyopokelewa kwa njia moja, Khabar-ul-Aahaad?

Huoni Ruduud alizochapwa zilizoandikwa na muheshimiwa Shaykh Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy katika kitabu kinachoitwa “Majmuu´-ur-Ruduud ´alaa Abiy-Hasan”?

Hujaona jinsi anavyounda kanuni kwa ajili ya kuwatetea Ahl-ul-Bid´ah?

Hujaona kuwa ameandika kitabu ambapo amewatetea Ahl-ul-Bid´ah na viongozi wao? Kina mijaladi miwili na kinaitwa “ad-Difaa´ ´an Ahl-il-Bid´ah”.

Hujui kuwa amejitenga mbali na Ahl-us-Sunnah wa Yemen na kuwatuhumu kuwa ni wagonjwa?

Hujui kuwa alisema kiherufi kwamba mfumo wa Shaykh Rabiy´ al-Madkhaliy – ambao ni mfumo wa Salaf na unakubaliwa na wanachuoni wakubwa akiwemo Shaykh al-Albaaniy – ni wenye kufutwa? Wakati Abul-Hasan alipoulizwa “Ni kwa nini hukuzungumzia hilo kabla ya kuzuka kwa fitina? Ni kwa nini hukubainishia tangu hapo kabla ya kwamba Shaykh Rabiy´ na watu hawa wana misingi mibovu” akajibu kwa kusema:

“Misingi ya Shaykh Rabiy´ imefutwa kwenye [kitabu changu] “as-Sirraaj al-Wahhaaj” tangu 1418.”

Kutokamana na kanuni zake mbovu Abul-Hasan amewashughulisha watu na:

1- Maelezo yaliyopokelewa kwa njia moja, Khabar-ul-Aahaad, yanafidisha dhana na si elimu.

2- Maneno ya kijumla ya watu yanatakiwa kufasiriwa na maneno yao maalum.

3- “Mtu anatakiwa kunasihi pasi na kuvunja.”

4- “Tutakuwa na mfumo mpana ambao wanaingia ndani yake Ahl-us-Sunnah wote na Ummah mzima.”

5- “Hatufuati kichwa mchunga.”

6- “Hakuna ambaye yuko na leseni katika Da´wah. Da´wah haihitajii kuwa na walinziwa milango.”

Malengo ya yote haya ni kushambulia mfumo wa Salaf na kuwaangusha wanachuoni wake. Pamoja na hivyo Allaah amemwangusha na fikira zake hazikufanikiwa. Vipi anaweza kutupilia mbali ukosoaji wa wanachuoni uliojengeka juu ya dalili na hoja kwa sababu anadai kwamba wanamfuata kipofo Shaykh Rabiy´? Uhakika wa mambo ni kwamba hauna lolote na ufuataji wa kipofu. Abul-Hasan:

1- Amewatukana Maswahabah alipowaita kuwa ni “povu.”

2- Amewalezea baadhi ya Mitume kwa njia ya kwamba ni wenye haraka ya kulaumu.

3- Amewatukana Maswahabah pindi aliposema kuwa malezi yao yana kasoro.

4- Ana kanuni mbovu na utata batili kwa njia ya kwamba anazituhumu dalili kwamba “sio muhimu” “zenye kutia khofu” na “jeruhi zisizokuwa na sababu”.

Tazama ambavyo anawachochea vijana na wapumbavu dhidi ya wanachuoni na kuwafanya kutupilia mbali hukumu zao pale ambapo anawatuhumu kwa dhulumu ya kwamba wanazungumza kutokamana na propaganda iliyojificha. Ameyafanya hayo baada ya kutokea mgawanyiko.

Hivi unajua kuwa Abul-Hasan mara nyingi ameita katika mgawanyiko na kuusifu? Ni mara ngapi wenye kujitolea Yemen na Saudi Arabia walijitahidi kuzima vurugu na kuzuia mpasuko, lakini kutamani kwake kuovu na propaganda zake za wazi na zilizojificha zinamfanya kushikamana na tofauti, mgawanyiko na vurugu.

Unajua kuwa ana mikanda zaidi ya 80 ilio na vita dhidi ya Ahl-us-Sunnah na fitina? Ukiongezea juu ya hilo uchokozi wake na wa wafuasi wake na yanayowekwa kwenye intaneti.

Hujasoma jinsi al-Maghraawiy anavyonukuu kutoka kwenye mikanda yake wakati anapowakufurisha waislamu?

  • Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: ad-Durar an-Najmiyyah fiy Radd-ish-Shubuhaat al-´Aqadiyyah wal-Manhajiyyah, uk. 388-391
  • Imechapishwa: 18/03/2017