Mwenye kukaa I´tikaaf kumtembelea mgonjwa na kwenda mazishini

Swali: Je, inajuzu kwa mwenye kufanya I´tiqaaf kumtembelea mgonjwa au kushuhudia jeneza? Baadhi ya wanazuoni wamesema haijuzu isipokuwa kama aliweka sharti kabla ya kuanza I´tiqaaf.

Jibu: Kama mgonjwa yupo ndani ya msikiti, basi hakuna tatizo kumtembelea. Kama swalah ya jeneza inaswaliwa msikitini, hapana shida kushuhudia. Lakini kama mgonjwa yuko nje ya msikiti au jeneza liko nje, basi haendi. Sunnah kwa mwenye kukaa I‘tiqaaf ni kutomtembelea mgonjwa aliye nje ya msikiti wala kutoshuhudia jeneza lililo nje ya msikiti, isipokuwa kama vyote viwili vipo ndani ya msikiti wake.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1248/حكم-زيارة-المعتكف-للمريض-وشهوده-الجنازة
  • Imechapishwa: 13/02/2026