Mwenye janaba kusoma Aayah al-Kursiy kabla ya kulala

Swali: Mtu ambaye anataka kulala hali yuko katika janaba asome Aayah al-Kursiy?

Jibu: Hapana, atasoma du´aa za kujikinga za Kishari´ah bila Aayah al-Kursiy, an-Naas, al-Falaq na al-Ikhlaasw. Ikiwa atapenda kufanya hivyo, basi aoge, kwani hilo ni bora zaidi kwake.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31530/هل-يقرا-الجنب-اية-الكرسي-عند-النوم
  • Imechapishwa: 01/11/2025