Je, viwanja vya ´iyd vinahesabiwa kuwa ni msikiti?

Swali: Misikiti ya ´Iyd siku hizi imezungushiwa uzio na kufichwa kwa watu. Je, inahesabiwa kuwa misikiti?

Jibu: Hilo ni kwa ajili ya kushika tahadhari na kutoka katika tofauti za wanazuoni, nalo ni jambo zuri ili asitwezwe na kusitupwe humo kitu katika chochote. Hivyo ni kwa ajili ya uangalifu na kwa lengo la kuchuka tahadhari na kujitakasa kwa ajili ya watu. Ama kuhusu kuhesabiwa kuwa ni msikiti unaohitaji kuswali Tahiyyat-ul-Masjid au kwamba ni haramu kukaa humo kwa mwenye janaba au mwenye hedhi, hilo linahitaji kutazamwa vizuri. Lakini kuiweka katika usafi na kuilinda dhidi ya uchafu ni jambo zuri na muhimu.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31532/هل-تعتبر-مصليات-العيد-مساجد-ولها-حكمها
  • Imechapishwa: 01/11/2025