Swali: Maswahabah walikuwa wakijipaka manukato walipokuwa wakikwenda kuswali, jambo ambalo ni sababu miongoni mwa sababu za kusaidia kupata unyenyekevu. Je, inajuzu kwangu mimi mwanamke kujitia manukato ninaposwali nyumbani?

Jibu: Hakuna ubaya katika hilo ikiwa hakuna mwanaume asiye Mahram kwako.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/125)
  • Imechapishwa: 02/03/2026