Mwanamke asimamishe ´ibaadah anapohisi alama za hedhi?

Swali: Wakati mwingine mwanamke anaweza kuhisi alama za kupata ada yake ya mwezi. Je, akihisi alama hizi za kupata hedhi aswali au asimamishe kuswali?

Jibu: Hukumu imefungamana na damu. Akitokwa na damu ndio asimamishe kuswali. Lakini midhali hajatokwa na damu yeye ni msafi. Hivyo aswali.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (09) http://audio.islamweb.net/audio/index.php?page=FullContent&audioid=191370#219699
  • Imechapishwa: 22/03/2019