Swali: Ikiwa mwanamume ameoa mke wa pili na yule mke wa kwanza akakataa kulala naye usiku au kukaa naye kisha baadaye akakubali. Je, mume ampe zamu yake?
Jibu: Amlazimishe mwanamke huyo.
Swali: Lakini ampe zamu yake au hakuna haja?
Jibu: Mwanamke huyo analazimika kunyenyekea hukumu ya Shari´ah na aridhie ugavi wa Allaah. Ni mamoja wake ni wawili, watatu au wanne. Mwanamke huyo akikataa hatopewa zamu. Haki yake itaanguka. Yeye ndiye ambaye amedondosha haki yake. Hatogawanyiwa chochote.
Swali: Akitoa zawadi ya siku yake kisha baadaye akaitaka?
Jibu: Anayo haki ya kuitaka tena. Amwambie ampe haki yake au amtaliki, kwa sababu pengine asiweze kusubiri.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23896/هل-للزوجة-طلب-استرجاع-حقها-الذي-اسقطته
- Imechapishwa: 29/05/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket