Swali: Ni ipi hukumu mume akisema kumwambia mke:
“Ni sawa ukitaka kubaki na watoto wako. Vinginevyo nenda kwa familia yako na huna lolote kuhusiana na mimi.”?
Jibu: Akimpa khiyari namna hii ameitakasa dhimma yake. Kwa ajili hii Sawdah bint Zam´ah (Radhiya Allaahu ´anhaa), ambaye ni mmoja katika mama wa waumini, wakati alipokhofia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) asije kumtaliki alimzawadia zamu yake ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ili apate kubaki pamoja na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ikawa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anamgawia ´Aaishah siku yake na ile siku ya Sawdah. Mwanaume huyu akimpa khiyari na kumwambia kwamba hawezi kufanya uadilifu baina yao; ima unisamehe na nitakasike, nikutaliki, nikuruhusu kwenda kwa familia yako na mfano wa hayo. Yakipatikana mambo hayo imetakasika dhimma yake.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Nuur ´alaad-Darb (13) http://binothaimeen.net/content/6779
- Imechapishwa: 09/02/2021
Swali: Ni ipi hukumu mume akisema kumwambia mke:
“Ni sawa ukitaka kubaki na watoto wako. Vinginevyo nenda kwa familia yako na huna lolote kuhusiana na mimi.”?
Jibu: Akimpa khiyari namna hii ameitakasa dhimma yake. Kwa ajili hii Sawdah bint Zam´ah (Radhiya Allaahu ´anhaa), ambaye ni mmoja katika mama wa waumini, wakati alipokhofia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) asije kumtaliki alimzawadia zamu yake ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ili apate kubaki pamoja na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ikawa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anamgawia ´Aaishah siku yake na ile siku ya Sawdah. Mwanaume huyu akimpa khiyari na kumwambia kwamba hawezi kufanya uadilifu baina yao; ima unisamehe na nitakasike, nikutaliki, nikuruhusu kwenda kwa familia yako na mfano wa hayo. Yakipatikana mambo hayo imetakasika dhimma yake.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Nuur ´alaad-Darb (13) http://binothaimeen.net/content/6779
Imechapishwa: 09/02/2021
https://firqatunnajia.com/mume-anamtilia-uwazi-mmoja-katika-wakeze-kwamba-hawezi-kufanya-uadilifu-2/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)