Swali: Ni ipi hukumu juu ya mtu anayemtilia shaka mke wake? Nini anachotakiwa kufanya?

Jibu: Haitakiwi kwake kujali shaka. Lakini akiona kwake alama za kutoshikamana na kujichunga na machafu na haramu… kwa mfano anachungulia kutoka dirisha moja kwenda dirisha jengine na mume akawa anajua kuwa mwanamke huyu amepewa mtihani na wanaume. Vinginevyo hatakiwi hatakiwi kumtilia shaka. Na ikitokea amemtilia shaka asijiaminishe. Hata hivyo haijuzu kumtuhumu kuwa ni mzinzi. Isipokuwa pale ambapo atamfumania na mwanaume akiwa juu yake na kijiko ndani ya kikombe au yeye mwenyewe mwanamke akakiri.

  • Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 245-246
  • Imechapishwa: 15/02/2025