Swali: Je, inajuzu kwa aliye katika Ihraam kufunika uso wake?
Jibu: Sahihi ni kwamba asifunike, kwa sababu katika Hadiyth Swahiyh ya kisa cha yule aliyekanyagwa na mnyama wake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Wala msifunike kichwa chake wala uso wake, kwani atafufuliwa siku ya Qiyaamah hali ya kuwa ni mwenye kufanya Talbiyah.”
Swali: Je, imepokelewa kutoka kwa Salmaan kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akifunika uso wake?
Jibu: Imepokelewa kutoka kwa ´Uthmaan, lakini Hadiyth Swahiyh inajulisha kukataza.
Swali: Lakini kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) imepokelewa kwa njia ya Hadiyth ya Salmaan?
Jibu: Sijui, bali iliyokuja ni kwa njia ya ´Uthmaan.
Swali: Kwa maana yeye ndiye alifanya hivo?
Jibu: Ndio, ni katika kitendo cha ´Uthmaan.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31075/هل-للمحرم-ان-يغطي-وجهه
- Imechapishwa: 02/10/2025
Swali: Je, inajuzu kwa aliye katika Ihraam kufunika uso wake?
Jibu: Sahihi ni kwamba asifunike, kwa sababu katika Hadiyth Swahiyh ya kisa cha yule aliyekanyagwa na mnyama wake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Wala msifunike kichwa chake wala uso wake, kwani atafufuliwa siku ya Qiyaamah hali ya kuwa ni mwenye kufanya Talbiyah.”
Swali: Je, imepokelewa kutoka kwa Salmaan kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akifunika uso wake?
Jibu: Imepokelewa kutoka kwa ´Uthmaan, lakini Hadiyth Swahiyh inajulisha kukataza.
Swali: Lakini kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) imepokelewa kwa njia ya Hadiyth ya Salmaan?
Jibu: Sijui, bali iliyokuja ni kwa njia ya ´Uthmaan.
Swali: Kwa maana yeye ndiye alifanya hivo?
Jibu: Ndio, ni katika kitendo cha ´Uthmaan.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31075/هل-للمحرم-ان-يغطي-وجهه
Imechapishwa: 02/10/2025
https://firqatunnajia.com/muhrim-asifunike-uso-wake/