Swali: Baadhi ya watu wanasema kuwa Muhaddithuun hawana uelewa; na kwamba fahamu zao ni za juujuu na kwamba ufahamu wa Fuqahaa´ ndio wenye kuingia kwa ndani. Unasemaje juu ya hilo? Haya yanasemwa na baadhi ya wanafunzi.
al-Albaaniy: Wanaosema maneno haya wao wenyewe ni Fuqahaa´?
Muulizaji: Sidhani hivo.
al-Albaaniy: Hapana shaka kwamba wao sio Fuqahaa´. Bali ni wajinga. Hebu wape baadhi ya mambo ya kisasa kisha utaona namna watakavoyafumbua. Hakuna faida kubwa ya kuraddi uchokozi wa watu hawa. Ni kuwarejesha katika msingi; wakiitikia ni sawa na la sivyo tunawaambia:
قُل لَّا تُسْأَلُونَ عَمَّا أَجْرَمْنَا وَلَا نُسْأَلُ عَمَّا تَعْمَلُونَ
“Sema: “Hamtoulizwa juu ya ule uhalifu tulioufanya na wala hatutoulizwa kwa yale mnayoyatenda.”[1]
[1] 34:25
- Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Raabigh (7) Dakika: 00:30
- Imechapishwa: 22/06/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)