Swali: Je, Malaika wawili, Munkar na Nakiyr, wanamuuliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kaburini mwake kama wanavyowauliza wengine?

Jibu: Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ametueleza kwamba kila maiti huulizwa kuhusu Mola wake, kuhusu dini yake na kuhusu Mtume wake. Hakutueleza kuhusu yeye mwenyewe (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Allaah ndiye anajua zaidi.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/2581/سوال-منكر-ونكير-للنبي-صلى-الله-عليه-وسلم-في-قبره
  • Imechapishwa: 28/03/2026