Swali: Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) si amezikwa ndani ya msikiti?

Jibu: Nyumbani kwa ´Aaishah na nyumba baadaye ikaingizwa ndani ya msikiti.

Swali: Kwa hivyo haisemwi kuwa yuko ndani ya msikiti?

Jibu: Hapana, haisemwi hivo. Yuko ndani ya nyumba. Lakini baadaye al-Waliyd bin ´Abdil-Malik alipopanua msikiti ndipo akaingizwa ndani. Alikosea kufanya hivo. Hata hayuko ndani ya msikiti. Nyumba ndio iko ndani ya msikiti. Nyumba ni yenye kujitegemea.

Swali: Vipi kuba?

Jibu: Kuba iliwekwa na baadhi ya waturuki waliokuja baadaye katika karne ya tisa au ya kumi. Ni kosa pia walilofanya.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24583/ما-الصواب-في-موضع-قبر-الرسول-ﷺ
  • Imechapishwa: 07/11/2024