Mtu Ananufaika Baada Ya Kufa Kwa Vitabu Alivyoacha?

Swali: Nikinunua misahafu, vijitabu, vipeperushi au vitabu vya elimu na nikavitawanya inaingia katika Hadiyth isemayo:

“Anapofariki mwanaadamu hukatika matendo yake isipokuwa vitu vitatu; swadaqah yenye kuendea, elimu yenye kunufaika kwayo au mtoto mwema mwenye kumuombea”?

Jibu: Ndio, vinaingia humo. Ukinunua vitabu vyenye manufaa na ukavitawanya inaingia katika elimu yenye kunufaika kwayo.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Fath-il-Majiyd (35) http://alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/fathul%20majid%20-%208%20-%201%20-%201437.mp3
  • Imechapishwa: 12/02/2017