Mtoto aliyenyonya maziwa ya mwanamke kutoka kwenye kikombe anahesabiwa ni mtoto wake?

Swali: Mwanamke alimnyonyesha mtoto kwa muda wa siku saba, lakini kunyonyesha hakukuwa moja kwa moja kutoka kifuani bali aliweka katika kikombe kisha mtoto akanywa. Je, unonyeshaji huu unahesabika?

Jibu: Hakuna tatizo, hapana neno. Kunyonyesha kunaweza kuwa kutoka kifuani moja kwa moja au kupitia chupa ya kunyonya. Kwa kuwa mara nyingine mtoto anakataa kunyonya moja kwa moja. Basi iwapo atanyonya mara tano au zaidi basi anahesabiwa kuwa mtoto wa kunyonyeshwa wa mwanamke huyo. Lakini sharti ni kuwa iwe ndani ya miaka miwili kabla ya kuachishwa ziwa.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31002/هل-ارضاع-المولود-من-كاس-يترتب-عليه-التحريم
  • Imechapishwa: 21/09/2025