Swali: Ni ipi hukumu ya swalah ya ambaye anaswali peke yake nyuma ya safu lakini akaja mwingine na kuswali naye?
Jibu: Ikiwa amejiunga naye katika Rak´ah ya kwanza basi inasihi swalah zao wote wawili. Na ikiwa wameshaswali Rak´ah moja basi aikate na kuianza swalah yake kuanzia pale ambapo alikuja mtu mwingine kujiunga naye ili swalah yake isihi.
Swali: Inasihi ile Takbiyrat-ul-Ihraam?
Jibu: Ndio, inasihi mpaka atakaporukuu. Akisharukuu na asije yeyote inabatilika, kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliikubali Rak´ah ya Abiy Bakrah aliyojiunga nje ya safu kisha baadaye ndio akajiunga na safu.
Swali: Je, inafaa kwa mtu anayeswali peke yake nyuma ya safu kumvuta mswaliji aliyeko safu ya mbele?
Jibu: Haifai kwake kufanya hivo.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23796/حكم-من-صلى-منفردا-ثم-اتى-شخص-معه
- Imechapishwa: 04/05/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)