Msikiti wa karibu au wa mbali zaidi?

Swali: Katika hatua za kutembea kwenda kuswali, ni bora kwenda msikiti ulio karibu na nyumba au ule ulio mbali?

Jibu: Kama msikiti wa karibu umenyooka na kundi lake la kuswali limenyooka, basi kila sehemu iliyo mbali zaidi huwa na fadhilah zaidi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”Watu wenye malipo makubwa zaidi katika swalah ni wale walio mbali zaidi kwa kutembea.”

Hivyo msikiti wa mbali zaidi ndio bora muda wa kuwa kwenda kwake katika msikiti huo wa mbali hakuleti madhara juu ya msikiti wa karibu, kuharibu swalah ya mkusanyiko wala kukuletea shida. Katika hali hiyo hakuna tatizo kwenda msikiti wa mbali zaidi kwa ajili ya kupata malipo zaidi kwa wingi wa hatua za kutembea.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1172/افضلية-الصلاة-في-المسجد-البعيد
  • Imechapishwa: 01/02/2026