Swali: Nini maana ya maneno yake kwamba anatubia kwa Allaah na kwa Mtume Wake?
Jibu: Ikiwa haki ni ya kiumbe basi mtu anatakiwa kutubia kwake kwa maana ya kwamba akaomba udhuru. Naomba udhuru kwa Allaah, Mtume Wake na kwa viumbe Wake. Imekuja katika tamko jengine:
“Natubia kwa Allaah na situbii kwa Muhammad.”
Akasema:
“Umeitambua haki kwa mwenye nayo.”
Swali: Na (الواو) hapa si inakuwa ya ushirika?
Jibu: Hapana. Maana yake ni kwamba natubia kwa Allaah kutokana na haki Yako na natubia kwako kutokana na haki yako, ee Mtume wa Allaah.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23867/معنى-واتوب-الى-رسوله-في-الحديث
- Imechapishwa: 23/05/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket