Swali: Wakati msafiri alipoingia msikitini na akawakuta watu wanaswali Dhuhr, akamwacha imamu kwanza aswali Rak´ah mbili kisha baadaye ndio akajiunga na imamu katika zile Rak´ah mbili za mwisho. Je, kitendo chake ni sahihi au si sahihi?
Jibu: Si sahihi. Ni wajibu kwake kuswali swalah ya imamu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Msikhitilafiane na maimamu wenu.”
“Hakika mambo yalivyo imamu amewekwa ili afuatwe.”[1]
Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ‘anhumaa) alipoambiwa kwamba baadhi ya watu wanaswali Rak´ah nne pamoja na imamu katika Haram na Rak´ah mbili wanapokuwa kwenye mahema yao huko Abtah, akasema:
“Hiyo ndio Sunnah ya Mtume wenu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”
Kwa hivyo maoni sahihi ni kwamba ni wajibu kumfuata imamu. Imamu akiswali Rak´ah nne, basi naye aswali Rak´ah nne. Msafiri amfuate imamu wake ambaye ni mkazi. Akiona kuwa imamu wake amekosea ataswali Rak´ah mbili na kumaliza kwa Sujuud mbili za kusahau.
[1] al-Bukhaariy (688) na Muslim (412).
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 298-299
- Imechapishwa: 27/04/2025
Swali: Wakati msafiri alipoingia msikitini na akawakuta watu wanaswali Dhuhr, akamwacha imamu kwanza aswali Rak´ah mbili kisha baadaye ndio akajiunga na imamu katika zile Rak´ah mbili za mwisho. Je, kitendo chake ni sahihi au si sahihi?
Jibu: Si sahihi. Ni wajibu kwake kuswali swalah ya imamu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Msikhitilafiane na maimamu wenu.”
“Hakika mambo yalivyo imamu amewekwa ili afuatwe.”[1]
Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ‘anhumaa) alipoambiwa kwamba baadhi ya watu wanaswali Rak´ah nne pamoja na imamu katika Haram na Rak´ah mbili wanapokuwa kwenye mahema yao huko Abtah, akasema:
“Hiyo ndio Sunnah ya Mtume wenu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”
Kwa hivyo maoni sahihi ni kwamba ni wajibu kumfuata imamu. Imamu akiswali Rak´ah nne, basi naye aswali Rak´ah nne. Msafiri amfuate imamu wake ambaye ni mkazi. Akiona kuwa imamu wake amekosea ataswali Rak´ah mbili na kumaliza kwa Sujuud mbili za kusahau.
[1] al-Bukhaariy (688) na Muslim (412).
Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 298-299
Imechapishwa: 27/04/2025
https://firqatunnajia.com/msafiri-amfuate-imamu-wake-mkazi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
