Msafiri amerejea nyumbani kwa mke wakati wa Ramadhaan

Nilimuuliza Ahmad:

”Unasemaje juu ya mtu ambaye amerejea nyumbani kwa mkewe katika Ramadhaan wakati wa mchana na mke wake pia hakufunga kwa sababu ya hedhi yake.” Akasema: ”Sipendelei amjamii. Ajizuilie kumjamii wakati anaporejea nyumbani kutoka safarini.”

Ishaaq amesema vivyo hivyo kama Ahmad na akaongeza:

”Akijamii mchana basi hatolazimika kutoa kafara.”

Ishaaq pia amesema vivyo hivyo.

  • Muhusika: Imaam Ishaaq bin Mansuur al-Kawsaj al-Marwaziy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Masaa-il-ul-Imaam Ahmad bin Hanbal wa Ishaaq bin Raahuuyah (667)
  • Imechapishwa: 01/03/2025