Swali: Je, ni lazima mbinu za kulingania ziwe kwa mujibu wa Qur-aan na Sunnah au ni kutokana na Ijtihaad ya mtu mwenyewe?
Jibu: Haijalishi kitu, hatutakiwi kwenda kunyume na dalili kwa maoni yetu. Inafaa kwa mlinganizi kulingania muda wa kuwa haendi kinyume na Qur-aan na Sunnah. Anaweza kulingania wakati wowote anaotaka kwa sharti asiendi kinyume na Qur-aan na Sunnah. Ulingano ambao unaenda kinyume na Qur-aan na Sunnah Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) haubariki. Allaah (´Azza wa Jall) amemwambia Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
ادْعُ إِلَىٰ سَبِيلِ رَبِّكَ بِالْحِكْمَةِ وَالْمَوْعِظَةِ الْحَسَنَةِ ۖ وَجَادِلْهُم بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ
“Lingania katika njia ya Mola wako kwa hekima na mawaidha mazuri na jadiliana nao kwa ambayo ni mazuri zaidi.”[1]
Ikiwa hekima ni kunyamaza, basi anyamaze, na ikiwa ni kuzungumza, basi azungumze:
قُلْ هَـٰذِهِ سَبِيلِي أَدْعُو إِلَى اللَّـهِ ۚ عَلَىٰ بَصِيرَةٍ أَنَا وَمَنِ اتَّبَعَنِي
“Sema: “Hii ndio njia yangu: nalingania kwa Allaah, juu ya ujuzi na umaizi – mimi na anayenifuata.”[2]
Lakini asiingize ndani ya ulinganizi yasiyokuwemo, kama mfano wa maigizo na mfano wake. Baadhi ya walinganizi wasiokuwa na elimu ya Qur-aan na Sunnah wanasema kuwa mtu asiwazungumzishe watu kwa Aayah za Qur-aan na Hadiyth za kinabii; wazungumzishe kutoka kichwani mwako. Hilo ni kwa sababu amekosa elimu ya Qur-aan na Sunnah.
[1] 16:125
[2] 12:108
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 396-397
- Imechapishwa: 23/06/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket