Swali: Je, haijuzu kwa mwanamke kumsusa mumewe?

Jibu: Haijuzu kwake kumhama mume wake. Akimsusa analaaniwa na Malaika mpaka kupambazuke; isipokuwa ikiwa ni kwa haki. Ikiwa ni kwa haki anadai haki yake. Akimfanyia mapungufu katika haki yake atoke kwenda kwa familia yake na kuomba haki yake. Lakini ikiwa anatekeleza haki yake haijuzu kwake kufanya hivo. Kwa ajili hiyo ndio Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akawakasirikia wakeze walipofanya waliyoyafanya katika mambo yaliyopelekea yeye kuwasusa. Alikasirika (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23887/هل-يجوز-للمراة-ان-تهجر-زوجها
  • Imechapishwa: 25/05/2024