Tambua kwamba watu wengi hii leo ni Ashaa´irah. Madhehebu yao inapokuja katika sifa za Mola (Subhaanahu wa Ta´ala) ni yenye kuafikiana na Mu´tazilah na Jahmiyyah.Wanathibitisha baadhi ya sifa tofauti na zengine.Wanathibitisha:
1- Uhai.
2- Elimu.
3- Uwezo.
4- Matakwa.
5- Kuona.
6- Kusikia.
7- Maneno.
Sifa zengine zote mbali na hizi wanazikanusha kwa upindishaji ambao ni batili. Pamoja na kwamba wanaafikiana na Ahl-us-Sunnah katika kuthibitisha sifa ya maneno, uhakika wa mambo ni kwamba wanaikanusha. Kwa sababu maneno kwa mtazamo wao ni maana peke yake. Aidha wanasema kuwa herufi za Qur-aan zimeumbwa na kwamba Allaah hazungumzi kwa herufi wala sauti. Jahmiyyah wanasema kwamba hayo ndio ambayo pia wao wanasema pindi wanapodai kwamba Qur-aan imeumbwa, wanachokusudia ni herufi na sio ile maana.
Ahl-us-Sunnah wote wanasema kwamba maneno ya Allaah hayakuumbwa, kwamba Allaah amezungumza kwa Qur-aan kwa herufi na maana na kwamba Allaah (Subhaanah) anazungumza kwa suati inayosikika na yule Anayemtaka.
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdullaah bin ´Abdir-Rahmaan Abaa Butwayn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ar-Rasaa-il wal-Masaa-il an-Najdiyyah (2/176-177)
- Imechapishwa: 14/03/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)