Swali: Je, inajuzu kwa mlinganizi kusema:
“Ee Allaah! Hakika mimi nakuomba kwa majina na sifa Zako kuu.”?
Je, du´aa hii huku ni kuiomba sifa?
Jibu: Nakuomba kwa majina mazuri kabisa na sifa Zako kuu, huku ni kutawassul kwa Allaah kwa majina na sifa Zako. Sio kuomba sifa. Ni kumuomba Allaah. Amesema (Ta´ala):
وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا ۖ وَذَرُوا الَّذِينَ يُلْحِدُونَ فِي أَسْمَائِهِ ۚ سَيُجْزَوْنَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ
”Allaah ana majina mazuri mno, hivyo basi muombeni kwayo na waacheni wale wenye kupondoka katika kuyapotosha majina Yake, watalipwa yale waliyokuwa wakiyatenda.”[1]
Hiyo “kwa” (باء) ni Tawassul. Ni kama mfano wa:
“Kwa rehema Zako nakuomba msaada.”
Hii ni Hadiyth.
Swali: Ni upi mfano uliokatazwa wa kuomba sifa ya Allaah?
Jibu: Kama vile kusema “Ee uso wa Allaah!”, “Ee rehema za Allaah!” na mfano wake.
[1] 07:180
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Nawaaqidh-il-Islaam, uk. 77
- Imechapishwa: 23/11/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket