Miongoni mwa ´Aqiydah ya Ahmad bin ´Abdillaah ni kwamba amesema:
“Yule mwenye kuamini kwamba ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh) atarejea ulimwenguni ni kafiri, na yule mwenye kusema kuwa Qur-aan imeumbwa ni kafiri.”
Imesemekana kwamba alikimbia magharibi ya Afrika wakati kulipotokea fitina ya kuumbwa kwa Qur-aan. Akafanya magharibi ya Afrika ndio makazi yake na akapata kizazi huko.
Yahyaa bin Ma´iyn aliulizwa kuhusu Ahmad bin ´Abdillaah bin Swaalih ambapo akajibu:
“Ni mwaminifu, mtoto wa mwaminifu.”
Baadhi yao wamesema kuwa Ahmad bin ´Abdillaah aliishi Tripoli ili aweze kupata faragha na kufanya ´ibaadah. Kaburi lake liko pwani na kaburi la mwanae liko pambizoni mwake. Ahmd al-´Ijliy amesema:
“Nilisafiri kwenda kwa Abu Daawuud at-Twayaalisiy. Akafariki siku moja kabla ya mimi kufika Baswrah.”
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Siyar A´laam-in-Nubalaa’ (12/506-507)
- Imechapishwa: 25/11/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)