Swali: Hadiyth:
”Hauondoi uchawi isipokuwa mchawi.”?
Jibu: Haya ni maneno ya baadhi ya Salaf, maneno ya al-Hasan (Rahimahu Allaah). Maana yake ni sahihi. Maana ya kwamba uchawi hauondolewi kwa yasiyokuwa matabano na dawa zinazokubalika katika Shari´ah. Isipokuwa mchawi ndiye anayeuondosha kwa kuwaabudia mashaytwaan. Hapana vibaya kuuondoa kwa matabano na dawa zinazokubalika katika Shari´ah. Miongoni mwa tiba bora ni zile du´aa za kinga za Kishari´ah:
أعوذ بكلمات الله التامات من شر ما خلق
“Najilinda kwa maneno ya Allaah timilifu kutokamana na shari ya alivyoviumba.”[1]
Aseme hivo asubuhi na jioni.
Asome Suurah ”al-Ikhlaasw”, ”al-Falaq” na ”an-Naas” mara kadhaa asubuhi na jioni na wakati wa kulala. Zote hizi ni miongoni mwa sababu za kujilinda.
[1] Muslim (2708).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24605/ما-صحة-مقولة-لا-يحل-السحر-الا-الساحر
- Imechapishwa: 12/11/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)